<a href="https://tracking.niji7.com/tracking?t=b7317bb9d043eae7299c1182c5b5581ab0498c197f70f2cb8f63f559040429cd&ap_id=5011&eco_id=1&link_id=1" class="niji7-affiliate" title="Japanese Used Cars | BE FORWARD"><span class="niji7-affiliate-text">Find Japanese Used Cars?</span></a>
wakubishiwa
Tuesday, October 23, 2018
Thursday, August 17, 2017
Tetesi za soka
TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 18.08.2017
Manchester United wanataka kumsajili kiungo wa Monaco Thomas Lemar. (Daily Record)
Manchester United bado wana matumaini ya kukamilisha usajili wa Ivan Perisic. (Mirror)
Tottenham wamefikia makubaliano ya kimsingi ya kumsajili Davinson Sanchez, 21, kutoka Ajax kwa pauni milioni 28 na milioni 14 zaidi kama marupurupu. (Independent)
Manchester City wapo tayari kuwapa West Brom pauni milioni 22 ili kumsajili nahodha wao Jonny Evans, 29, baada ya dau la pauni milioni 18 kukataliwa, na watampa mara mbili ya mshahara wa pauni 75,000 kwa wiki anaolipwa sasa. (Mirror)
Dau la Chelsea la pauni milioni 62 kumtaka beki wa Juventus Alex Sandro, limekataliwa. (Mirror)
Chelsea wanajiandaa kumuuza Diego Costa kwa hasara. (Sun)
Mkurugenzi wa michezo wa Barcelona Robert Fernandez amesema itakuwa “vigumu” kumsajili kiungo wa Liverpool Philippe Coutinho, 25, kwa sababu hana kipengele cha uhamisho kwenye mkataba wake. (Liverpool Echo)
Barcelona “watapigana” mpaka siku ya mwisho ya usajili ili kumsajili Philippe Coutinho kutoka Liverpool. (Telegraph)
Mshambuliaji wa Chelsea Diego Costa, 28, amesema hatorudi Stamford Bridge na anataka kujiunga na Atletico Madrid. (Telegraph)
Everton huenda wakamtaka Diego Costa kwa mkopo. (Sun)
Beki wa Tottenham Kevin Wimmer, 24, anazungumza na Stoke City kuhusu uhamisho wake wa pauni milioni 15. (Telegraph)
Stoke City pia wanataka kumsajili Kevin Wimmer kutoka Spurs. (Stoke Sentinel)
Beki wa Arsenal Gabriel, 26, anakaribia kujiunga na Valencia kwa pauni milioni 10. (Evening Standard)
Paris Saint-Germain bado wanataka kumsajili kiungo mkabaji wa Monaco, Fabinho, 23. (L’Equipe)
Kiungo wa PSG Blaise Matuidi, 30, amekamilisha vipimo vya afya Juventus, lakini timu hizo mbili bado hazijakubaliana jinsi ada ya uhamisho itakavyolipwa, huku meneja wa PSG Unai Emery akisema hakutaka kumuuza mchezaji huyo. (Le Parisien)
Wakurugenzi wa Borussia Dortmund wamesema Barcelona “hata hawapo karibu” katika kufikia dau la mshambuliaji wake Ousmane Dembele, 20. (Kicker)
Fiorentina wamemwambia mshambuliaji wake Nikola Kalinic, 29, anayenyatiwa na AC Milan kuwa atapigwa faini kwa kutotokea mazoezini siku ya Alhamisi. (Sun)
Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumaa Kareem.
Monday, August 14, 2017
Tetesi za soka ulaya
TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATATU 14.08.2017
Chelsea wanafikiria kutaka kumsajili mchezaji anayenyatiwa na Manchester United Ivan Perisic , 28, kutoka Inter Milan. (Mirror)
Barcelona wanataka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard, 26. (Diario Gol)
Cezar Azpilicueta, 27, anadhani Chelsea wanahitaji kusajili wachezaji kadhaa zaidi kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Evening Standard)
Chelsea wapo tayari kupanda dau la pauni milioni 50 wiki hii kumtaka beki wa kati wa Southampton Virgil van Dijk na kuwapiku Liverpool. (Daily Star)
Manchester United watakuwa tayari kulipa pauni milioni 36.5 kumsajili kiungo wa Barcelona Sergi Roberto, 25, ikiwa mchezaji huyo atataka kuondoka Uhispania. (Don Balon)
Manchester United wanakaribia kufikia makubaliano na Oliveirense ya Ureno kumsajili mshambuliaji Bruno Amorim, 19. (Daily Mail)
Antoinne Griezmann, 26, atachukizwa na hatua ya Atletico Madrid kumuuza kipa wake Jan Oblak na huenda akafikiria kuhamia Manchester United. (Don Ballon)
Leicester City watakataa dau la Roma la pauni milioni 31 la kumtaka Rirad Mahrez. Leicester wanataka pauni milioni 50. (Mirror)
Mkurugenzi mkuu wa Juventus Beppe Marotta amesema wanamtaka kiungo anayesakwa na Liverpool Naby Keita, 22, anayechezea RB Leipzig. (La Gazzetta dello Sport)
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp amesema anahitaji kuimarisha kikosi chake kabla ya dirisha la usajili kufungwa. (Liverpool Echo)
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp anafikiria kumsajili mshambuliaji wa Napoli Lorenzo Insigne, kuchukua nafasi ya Philippe Coutinho anayenyatiwa na Barcelona. (Express)
Barcelona hawatokata tamaa ya kumsajili Philippe Coutinho, 25, kutoka Liverpool, na wapo tayari kutoa pauni milioni 137 kumshawishi mchezaji huyo. (The Sun)
Mshambuliaji wa Real Madrid Marco Asensio atakuwa na mazungumzo ya dharura na klabu yake kuhusiana na kutaka kuhamia Arsenal. (The Mirror)
Tottenham wataongeza bidii ya kutaka kumsajili mshambuliaji wa Lazio Keita Balde, 22, ambaye hakupangwa katika kikosi cha kwanza kwenye mechi iliyopita. (Mirror)
Winga wa PSG Jese Rodriguez, 24, amekataa kwenda Fiorentina kwa mkopo na anajiandaa kwenda Stoke kwa mkopo. (Sun)
Schalke wanazungumza na Chelsea kuhusu kumchukua tena kwa mkopo beki Baba Rahman, 23. (Sky Sports)
Newcastle wameongeza bidii ya kujaribu kumsajili kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 25, baada ya mchezaji huyo kuachwa katika kikosi kilichocheza dhidi ya Leicester. (Sun)
Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki njema.
Sunday, August 13, 2017
Usajili ulaya
TETESI ZA SOKA ULAYA JUMAPILI 13.08.2017
Paris Saint-Germain wamekamilisha usajili wa Kylian Mbappe, 18, kutoka Monaco kwa pauni milioni 173. (The Times)
Real Madrid watawapiku Barcelona katika kumsajili mshambuliaji wa Borussia Dortmund Ousmane Dembele, 20. (RAC-1)
Manchester United wametupilia mbali dau la Tottenham la kumtaka Anthony Martial, 21. (RMC Sport)
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp atataka kumsajili mshambuliaji wa Napoli Lorenzo Insigne, 26, iwapo Philippe Coutinho, 25, atalazimisha kuondoka na kwenda Barcelona. (Sunday People)
Barcelona watarejea Liverpool na dau la pauni milioni 100 kumtaka Philippe Coutinho. (Sunday Express)
Chelsea wiki hii watapanda dau la pili la takriban pauni milioni 25 kumtaka kiungo wa Leicester City Danny Drinkwater, 27, baada ya pauni milioni 15 za awali kukataliwa. (Sunday Telegraph)
Real Madrid wamekiri kukata tamaa ya kutaka kumsajili kipa wa Manchester United David De Gea msimu huu. (Sunday Express)
Barcelona wamemsajili kiungo wa zamani wa Tottenham, Paulinho, 29, kwa pauni milioni 36.6 kutoka Guangzhou Evergrande ya China. (Mail on Sunday)
Paris Saint-Germain huenda wakatumia zaidi ya pauni milioni 54.9 kumsajili beki wa Monaco Fabinho, 23. (ESPN)
Kiungo Mjerumani Mesut Ozil, 28, hataki kubakia Arsenal na anataka kulazimisha uhamisho wa kwenda Barcelona. (Don Balon)
Tottenham watamwaga fedha kabla ya dirisha la usajili kufungwa, wakianza na kupanda dau la kumtaka kiungo wa Everton Ross Barkley, 23. (Sunday Telegraph)
Meneja wa Tottenham Mauricio Pochettino anahoji kwanini wanamfuatilia Ross Barkley, yeye anawataka zaidi kiungo wa Celta Vigo Pape Cheikh Diop, 20, na beki wa Ajax Davinson Sanchez, 21. (Sun on Sunday)
Ajax wamekataa dau la pauni milioni 36.6 kutoka Tottenham la kumtaka Davinson Sanchez, na amepewa mkataba mpya ili kumshawishi asalie Ajax. (De Telegraaf)
Chelsea watakuwa tayari kumuuza Eden Hazard, 26, iwapo Barcelona watakuwa tayari kutoa pauni milioni 110. (Diario Gol)
Manchester United wameanza tena mazungumzo na Inter Milan ya kutaka kumsajili winga Ivan Perisic, 28, na wanakaribia kutoa kitita cha pauni milioni 48 wanachotaka Inter. (Sunday Mirror)
Chelsea wana wasiwasi kuwa mshambuliaji wake Diego Costa, 28, amenenepa sana baada ya kwenda likizo ya mapumziko Brazil na huenda ikawa vigumu kumuuza. (Sunday Times)
Diego Costa huenda akapigwa faini na Chelsea kwa kushindwa kurejea mazoezini wiki mbili zilizopita. (Daily Star)
Liverpool wamemuambia Emre Can, 23, kuwa haendi popote licha ya Juventus kujipanga kutoa pauni milioni 23 kumtaka kiungo huyo Mjerumani ambaye amebakiza mwaka mmoja kwenye mkataba wake. (Sunday Mirror)
Kiungo wa Swansea Gylfi Sigurdsson, 27, hatimaye atakamilisha uhamisho wake kwenda Everton wiki hii, na hivyo kufanya Swansea kumfuatilia kiungo wa West Brom Nacer Chadli, 28, na huenda kusababisha Tottenham kumsajili Ross Barkley, 23, kutoka Everton. (Sunday People)
Meneja wa Everton Ronald Koeman, baada ya kumsajili Gylfi Sigurdsson atataka kumsajili mshambuliaji wa Fiorentina Nikola Kalinic, 29. (Sunday Express)
Mshambuliaji wa kimataifa wa Croatia na Fiorentina Nikola Kalinic, 29, anataka kwenda AC Milan. (Sky Sports)
Mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Antoinne Griezmann, 26, huenda akaondoka Atletico Madrid, iwapo kipa Jan Oblak, 24, atauzwa kwenda PSG. (Don Balon)
Kiungo mshambuliaji wa Real Madrid Marco Asensio, 21, anataka kutumia nafasi ya Arsenal kumnyatia ili apate mkataba mpya Real. (Diario Balon)
Arsenal wamekata tamaa ya kumsajili kiungo wa Monaco Thomas Lemar, 21, na sasa meneja Arsene Wenger anatazama zaidi kupunguza wachezaji asiowahitaji ili kupunguza gharama za mishahara. (Mail on Sunday)
Meneja wa Newcastle Rafael Benitez anataka kumsajili kiungo wa Arsenal Jack Wilshere, 25. (Sun on Sunday)
Tukutane baadaye katika BBC Ulimwengu wa Soka ambapo tutakutangazia mechi ya Manchester United v West Ham United.
Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumapili njema.
Friday, August 11, 2017
Tetesi za soka
TETESI ZA SOKA ULAYA IJUMAA 11.08.2017
Arsenal wamempa Alexis Sanchez mkataba mpya na mshahara wa pauni 300,000 kwa wiki na kumfanya mchezaji anayelipwa zaidi katika EPL. (Daily Mail)
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amekiri kuwa “hana uhakika sana” kama ataweza kumshawishi Alexis Sanchez kukubali kusaini mkataba mpya. (SFR)
Juventus wanajiandaa kutoa pauni milioni 23 kujaribu kuishawishi Liverpool kumuuza Emre Can. (Gazzetta dello Sport)
Juventus nao wameingia katika mbio za kutaka kumsajili Sergi Roberto kutoka Barcelona, ambaye pia Manchester United na Chelsea zinamtaka. (Sport.es)
West Ham wamepanda dau la pauni milioni 27.1 kumtaka kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 25. (Daily Telegraph)
Barcelona hawatakuwa na uwezo wa kumnunua Philippe Coutinho kutoka Liverpool iwapo watafanikiwa kumsajili Ousmane Dembele, 20, kutoka Borussia Dortmund, kwa mujibu wa mwandishi wa ha1ba12ri za michezo Graham Hunter. (BBC Radio 5 Live)
Barcelona wapo tayari kuwapa Liverpool Ivan Rakitic kama sehemu ya mkataba wa kumsajili Philippe Coutinho. (Don Balon)
Barcelona wanamtaka kiungo mchezeshaji wa Real Madrid Marco Asensio na wapo tayari kutoa pauni milioni 72. (Diario Gol)
Mwenyekiti wa Tottenham Daniel Lexy anakabiliwa na sekeseke la wachezaji kudai kuongezewa mishahara baada ya beki Danny Rose kushutumu sera za klabu hiyo. (Daily Mirror)
Danny Rose alipokelewa kwa shangwe na wachezaji wenzake baada ya kuweka wazi mtazamo wa Tottenham, huku wachezaji wengine wakitishia na wao kuweka mambo hadharani. (Daily Mirror)
Wachezaji nyota wa Tottenham wanataka kuondoka kwa sababu ya sera ya malipo ya klabu hiyo. (Daily Mail)
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anatafuta beki wa kushoto na Danny Rose wa Tottenham ni mmoja wa wachezaji anaowafuatilia. (Daily Record)
Meneja wa Everton Ronald Koeman ameiambia Tottenham kuwa hawataweza kumsajili kiungo Ross Barkley kwa bei rahisi. (Daily Star)
Arsenal wanaamini kuwa wamefanikiwa katika mazungumzo ya kumshawishi Mesut Ozil kubakia Emirates baada ya kumpa mkataba wa mshahara wa pauni 225,000 kwa wiki, na mchezaji huyo ameonesha dalili za kukubali. (Sun)
PSG wapo tayari kuwapa Atletico Madrid Javier Pastore katika mkataba wa kumsajili kipa Jan Oblak, 24. (AS)
Real Madrid wamekuwa na mazungumzo ya siri na Juventus kuhusiana na mshambuliaji Paulo Dybala, 23, ambaye pia anasakwa na Barcelona. (Don Balon)
Juventus wanamtaka Kevin Strootman kabla ya dirisha la usajili kufungwa, huku Roma wakisema bei yake ni euro milioni 45. (Tuttosport)
Arsene Wenger amesema meneja wa Chelsea Antonio Conte awarejeshe wachezaji wanaocheza nje kwa mkopo kama ana wasiwasi na idogo wa kikosi chake. (Times)
Msimu wa EPL unaanza rasmi leo. Arsenal wanacheza na Leicester City saa nne kasorobo usiku huu kwenye uwanja wa Emirates. Matokeo ya mchezo huo utayapata hapa hapa.
Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Jumaa Kareem.
Thursday, August 10, 2017
Tetesi za soka
TETESI ZA SOKA ULAYA ALHAMISI 10.08.2017
Meneja wa Manchester United Jose Mourinho anataka kusajili angalau mchezaji mmoja zaidi kabla ya dirisha la usajili kufungwa, huku beki wa kushoto Danny Rose, 27, na winga wa Inter Milan Ivan Perisic wakiendelea kunyatiwa na United. (Manchester Evening News)
Jose Mourinho ameitaka Manchester United kupanda dau la pauni milioni 100 kumtaka Gareth Bale wa Real Madrid. (The Sun)
Danny Rose amesema hana mpango wa kuondoka Tottenham, lakini anaamini anastahili kulipwa zaidi kuliko anavyolipwa sasa. (Sun)
Danny Rose ameitaka Tottenham kusajili wachezaji wenye majina makubwa. (Sun)
Tottenham wapo tayari kutoa pauni milioni 55 kumtaka beki wa Ajax Davinson Sanchez. (The Sun)
Paris Saint-Germain wanakaribia kumsajili mshambuliaji wa Monaco Kylian Mbappe, 18, kwa pauni milioni 163, na tayari wamekamilisha mkataba na Fabinho, 23, pia wa Monaco. (Daily Record)
Iwapo Kylian Mbappe ataondoka, Monaco wataamua kumfuatilia mshambuliaji wa kimataifa wa Colombia, Carlos Bacca anayeichezea AC Milan. (Caracol Radio)
Chelsea wamepanda dau la pauni milioni 35 kumtaka kiungo mshambuliaji wa Arsenal Alex Oxlade-Chamberlain, 23. (Daily Star)
Chelsea wanazidi kuonekana kuwa na nafasi zaidi ya kumsajili kiungo mshambuliaji wa Everton Ross Barlkey, ambaye pia ananyatiwa na Tottenham. (Daily Telegraph)
Arsenal wana wasiwasi kuwa mshambuliaji wake Alexis Sanchez, 28, huenda akataka kulazimisha uhamisho wake kuondoka Emirates. (Daily Mirror)
Barcelona watarejea tena Liverpool na dau la nne la kumtaka kiungo mshambuliaji kutoka Brazil Philippe Coutinho, 25. (Daily Mail)
Barcelona na Atletico Madrid wanapambana katika kutaka kumsajili Lautaro Martinez anayechezea Racing Club ya Argentina. (El Grafico)
Barcelona wameambiwa walipe pauni milioni 135 kama wanataka kumsajili Ousmane Dembele, 20, wa Borussia Dortmund. (the Guardian)
Meneja wa Liverpool Jurgen Klopp ndio kizingiti kikuu katika majadiliano yoyote kuhusu usajili wa Philippe Coutinho. (Marca)
Philippe Coutinho hatowasilisha maombi ya kutaka kuondoka Liverpool ili kulazimisha uhamisho wake. (Sport)
West Ham wanajiandaa kutoa dau la pauni milioni 25 kumtaka kiungo wa Sporting Lisbon William Carvalho, 25. (Daily Mail)
Kiungo wa Chelsea Willian, 29, alizungumza na Manchester United msimu huu kuhusu uwezekano wa kuhamia Old Trafford. (Goal)
Newcastle wamefanikisha usajili wa mkopo wa winga wa Chelsea, Kenedy, 21. (Daily Mirror)
Manchester United wameanza mazungumzo na Zlatan Ibrahimovic, 35, kuhusu mkataba mpya, wakati mchezaji huyo akiendelea kupata nafuu ya jeraha lake la goti. (Daily Mail)
Zlatan Ibrahimovic anaendelea na mazoezi na amemuambia Jose Mourinho kuwa anataka kubakia Old Trafford. (Guardian)
Meneja wa Marseille Rudi Garcia amesema mshambuliaji wa Arsenal Olivier Giroud, 30, “atawafaa sana” lakini mfaransa huyo hana mpamgo wa kujiunga na klabu hiyo ya Ligue 1. (L’Equipe)
Meneja wa Newcastle Rafael Benitez amezungumza na Arsene Wenger wa Arsenal kuhusu kutaka kumsajili Lucas Perez, 28, lakini Arsenal wameshikilia bei ya pauni milioni 13.4. (Chronicle)
Kiungo wa Real Madrid, Isco, 25, anakaribia kusaini mkataba mpya na hivyo kuwanyima nafasi Manchester United na Arsenal ya kumsajili. (Independent)
Meneja wa Chelsea Antonio Conte ameiambia bodi ya klabu yake kumsajili beki wa kulia wa Barcelona Sergi Roberto, 25. (Sport)
Beki wa Valencia Joao Cancelo, 23, anakaribia kujiunga na Chelsea. (Don Balon)
Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.
Wednesday, August 9, 2017
Usajili ulaya
TETESI ZA SOKA ULAYA JUMATANO 09.08.2017
Barcelona wanataka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Liverpool Philippe Coutinho, 25, ifikapo mwisho wa wiki hii. (Mirror)
Liverpool wamekataa kumuuza Coutinho licha ya maafisa wa Barcelona kwenda England kujadili uhamisho huo na wapo tayari kuongeza dau lao la pauni milioni 120. (Star)
Rais wa Real Madrid Florentino Perez amewaambia waandishi wa habari kuwa klabu yake haina mpango wa kumuuza Gareth Bale, 28, kufuatia Manchester United kumnyatia. (Star)
Katika mazungumzo ya faragha Florentino Perez amemuambia Jose Mourinho kuwa yuko tayari kumuuza Bale. (Diario Gol)
Meneja wa Chelsea ameitaka klabu yake kupanda dau kumtaka beki wa Tottenham Danny Rose, 27. (Sun)
Chelsea wanataka kumsajili Joao Cancelo kutoka Valencia. (Sky)
Manchester City wamemuulizia kiungo wa Barcelona Sergio Busquets, 29. (Onda Sera)
Inter Milan wamejiunga katika mbio za kutaka kumsajili kiungo mshambuliaji wa Leicester City Riyad Mahrez, 26, baada ya dau la pauni milioni 32, la Roma kukataliwa. Leicester wanataka pauni milioni 50. (Mirror)
Paris Saint-Germain wapo tayari kuwazidi kete Manchester City kwa kutoa pauni milioni 80 kumsajili mshambuliaji wa Arsenal Alexis Sanchez, 28. (Independent)
Kylian Mbappe, 18, ameamua kuwa anataka kwenda Paris Saint-Germain, huku PSG wakijiandaa kutoa euro milioni 155 kumsajili mchezaji huyo wa Monaco. (Telefoot)
Chelsea na Manchester United wamepewa ishara ya kumfuatilia beki wa kulia wa PSG Serge Aurier, 24, baada ya klabu hiyo kusema mchezaji huyo wa kimataifa wa Ivory Coast anauzwa. (Telegraph)
Southampton wako tayari kumuacha Virgil van Dijk “aozee benchi” kuliko kumuuza. (Express)
Mazungumzo ya Everton na Swansea kuhusu usajili wa Gylfi Sigurdsson yameporomoka. (Sky Sports)
Mshambuliaji wa Leicester City Ahmed Musa, 24, huenda akajiunga na Hull City. (Leicester Mercury)
Habari zilizothibitishwa tutakujuza mara zitakapothibitishwa. Kwa orodha kamili ya wachezaji waliokamilisha rasmi usajili bofya link hii: http://www.bbc.co.uk/sport/football/transfers
Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa. Uwe na wiki yenye tija na mafanikio.